Wino Mwekundu
Publisher
Uwaridi
Language
Swahili
BOOK OVERVIEW
Davina akiwa kwenye hatua za mwisho za kuingia kwenye ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi Chaka, anapata pigo. Chaka anafariki katika ajali mbaya ya gari. Linakuwa jambo lenye maumivu maishani mwake, lakini maumivu makubwa zaidi yanajitokeza baada ya kifo hicho. Chaka anamwandikia barua kwa kutumia kalamu yenye ‘Wino Mwekundu’. Ndani ya barua hiyo anapewa ujumbe wa kutisha na kuogofya. Chaka anamuahidi kumchukua na kwenda naye kuzimu. Huo unakuwa mwanzo wa misukosuko katika kisa hiki cha kusisimua, kilichoandikwa kwa ustadi mkubwa. Fuatilia...